Thursday, July 19, 2012

MH MKONO ATIMIZA AHADI YAKE YA MADAWATI KWA SEKONDARI YA BUTUGURI
 .Madawati yaliyotengenezwa na TASAF chini ya kiwango yarudishwa halamshauri ya Musoma
 Mmilikiwa wa Blog ya Mwana wa Afrika akiwa diwani wa Kata ya Butuguri na waandishiwa habari katika shule ya sekondari Butuguri kushuhudia madawati mapya yaliyoletwa na Mh NimroDI Mkono Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini
       Wanafunzi wa shule ya Sekondari Butuguri wakiwa katika moja ya darasa na kwenye madawati yaliyotengenezwa na Mh Mkono
                           Mwalimu akifundisha moja ya darasa lililotengenezwa na Mh Mkono
           Shule inaendelea kama kawaida
         Mwandishi wa ITV mkoani Mara akipata maelezo kutoka kwa Diwani wa Kata ya Butuguri Mh Mwita Charles
      Baadhi ya Madawati yaliyotengenezwa na TASAF yakiwa yameharibika muda mfupi tangu yatengenezwe
  Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Butuguri ( Geofrey Robert akihojiwa na Mwandishi wa ITV
                                  Madawati ya TASAF
                       Madawati yaliyotengenezwa na Mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Nimrodi Mkono
                                                              Madawati
                                                     Madawati mapya
                   Raha ya shule ni kusoma katika mazingira Bora
  Madawati yaliyotengenezwa na TASAF yakipakiwa ndani ya gari tayari kurudishwa Halmashauri
                       Madawati chini ya kiwango yakipakiwa ndani ya gari kupelekwa TASAF
     Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrodi Mkono akitazama baadhi ya madawati hivi karibuni na kubaini kuwa madawati hayo yaliyotengenezwa na TASAF kuonekana hayana kiwango


MUSOMA

MBUNGE  wa Jimbo la Musoma Vijijini Nimroadi Mkono amekamilisha ahadi yake ya kupeleka Madawati mapya katika shule ya sekondari Butuguri baada ya kubainika kuwa madawati yaliyotengenezwa na mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika shule hiyo hayana ubora.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea awamu ya kwanza ya Madawati zaidi ya 50,diwani wa kata ya Butuguri Mwita Charles alimpongeza Mbunge huyo  kwa kukamilisha ahadi hiyo huku akitoa wito kwa viongozi wengine kuiga mfano huo.

Diwani huyo alisema kuwa Madawati yaliyotengenezwa na TASAF hayana ubora na hivyo anaunga mkono kauli ya Mh Mbunge kuyarudisha Madawati hayo katika Halmashauri ya Musoma.

Kuhusu wale wote waliohusika katika ubadhilifu huo diwani huyo alisema kuwa wanatakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa viongozi wengine ambao wapo kwa masilahi yao.

Naye Mwalimu mkuu Wa Shule hiyo Godfrey Robert alisemshukuru Mbunge huyo na kusema kuwa amesaidia kupunguza mzigo kwa wazazi katika kukabiliana na upungufu wa madawati uliokuwepo shuleni hapo.

Amesema Madawati yaliyokuwepo hayatoshi ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi waliopo katika shule hiyo,na hivyo mwaka  huu walikuwa na mpango wa kutengeneza madawati hayo.

Aidha madawati yote yaliyotengenezwa na mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF tayari yamerudishwa katika halmashauri ya Musoma Vijijini kutokana na kutokuwa na kiwango kinachokubalika

Hivi karibuni akifanya ziara shuleni hapo mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrodi Mkono aliyakataa madawati zaidi ya 1000 yaliyotengenezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kutokana na kutokuwa na kiwango kinachokubaliwa

No comments:

Post a Comment