Maandamano
ya wananchi wa mji mdogo wa sirari wilaya ya Tarime mkoani Mara waliotaka kujua chanzo cha mauaji ya kijana
mmoja mkazi wa eneo hilo ambaye anadaiwa kukamatwa na Jeshi la polisi na kisha mwili
wake kukutwa katika chumba cha kuhifadhiwa maiti katika hospital ya wilaya ya
Tarime yamesababisha vurugu kubwa na kusimama kwa shughuli mbalimbali za
kijamii kwa saa kadhaa
Kijana huyo
aliyefahamika kwa jina la kitandika Ryoba anadaiwa kukamatwa siku nne
zilizopita na askari wa jeshi la Polisi katika mkoa wa kipolisi Tarime Rorya
kwa tuhuma za kukutwa akicheza kamali
lakini tangu siku ya tukio hilo kijana huyo hakupatikana hadi taarifa za
kifo zilipowafikia ndugu zake na mwili
wake kuhifadhiwa katika chumba cha Maiti katika hospital ya wilaya ya Tarime
Taarifa hizo
zilisababisha wananchi wa eneo hilo kufanya Maandamano ikiwa ni njia ya kushinikiza jeshi la Polisi kueleza chanzo cha kifo cha kijana huyo ambapo jeshi la polisi
liliingia kati kuzima maandamnao hayo hali ambayo ilisababisha wananchi hao kuifunga barabara
kuu ya inayotumika kwa safari za Mwanza,Tarime na nchi jirani ya Kenya kwa kutumia Mawe lakini pia wakichoma matairi
ya Magari.
Kwa upande wake
Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Tarime Rorya Kamishana msaidizi Mwandamizi
Justus Kamgisha amesema Mtuhumiwa huyo kitandika Ryoba baada ya kukamatwa
alifikisha kituo cha Polisi kuhojiwa na wakati Mahojiano yakiendelea alidai
kujisikia vibaya ambapo nalikimbizwa hospital na wakati anapatiwa matibau
akafariki dunia.
No comments:
Post a Comment