B w Onesmo Olengurumwa - Mratibu Wa Kitaifa Wa Mtandao
TAREHE 12/12/2013
KUHUSU SIKU YA WATETEZI
WA HAKI ZA BINADAMU
TANZANIA
Ndugu waalikwa, mabibi na
mabwana, mabalozi na wawakilishi wa baadhi ya balozi zilizopo nchini, familia
ya watetezi wa haki za binadamu, waaandishi wa habari na wageni wote waliakwa,
habari za asubuhi.
Mhe Mwenyekiti, Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) ni
Mtandao ambao unajumuisha watetezi wa haki za binadamu hapa nchini. Lengo la
Mtandao huu ni kujenga mazingira salama kwa watetezi kufanya kazi zao za
utetezi. Malengo
makuu ya Mtandao ni kama
ifuatayo.
a)
Mfumo wa kisheria, kisera na hata wa kiuzoefu, unaotambua na kulinda watetezi wa
haki za binadamu na utandaa/ushirikiano wa mashirika yasiyo ya kiserikali
kuboreshwa ( Uraghabishi/ Utetezi)
b)
Uwezo wa waandishi wa habari na watetezi wa haki za
binadamu umeongezeka na hivyo wanaweza
kushiriki kikamilifu katika michakato ya ulinzi kwa watetezi wa haki za
binadamu na kushughulikia haki za watetezi wa haki za binadamu (KUJENGA UWEZO).
c)
Utaratibu
wa ulinzi imara kupatikana kwa kuwaondoa watetezi katika hatari (USALAMA/ULINZI)
d)
Utendaji bora na endelevu kwa Mtandao wa
Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
(UJENZI
WA TAASISI)
Mhe
Mwenyekiti, Watetezi wanayo haki ya kulindwa na sheria za nchi husika pale
wanapokuwa wanatimiza majukumu yao.
Lakini utetezi huo usihusishe matumizi ya nguvu, na kitendo chochote cha
kutowalinda watetezi ni ni cha uvunjifu wa haki za binadamu. Mpaka sasa Tanzania bado
haijaridhia mikataba kadhaa ya kimataifa inayowatambua na kuwalinda watetezi wa
haki za binadamu katika mfumo wa sheria zake. Ni kwa sababu hiyo Mtandao wa
Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
umedhamiria kutumia njia za uraghabishi mbalimbali kupata mafanikio. Ili kukamilisha azma hii Mtandao huu umedhamiria
kuwakutanisha wadau mbali mbali katika ngazi ya kitaifa na ngazi ya
kimataifa. Zifuatazo ni baadhi ya
shughuli ambazo zimekamilishwa na mtandao huu katika muktadha huu:
Katika utekelezaji wa lengo la kwanza la
Mtandao (Advocacy) , Mtandao umeanzisha siku ya Watetezi Tanzania wa
Haki za Binadamu hapa nchini kwa lengo la kuongeza utambulisho na ulinzi wa
watetezi hapa nchini. Siku hii ya watetezi nchini ni tofouti na siku ya haki za
binadamu inayoazimishwa kila mwaka tarehe 10 Disemba. Siku hii ni mahususi kwa
ajili ya maslahi, haki na usalama wa watetezi wa haki za Binadamu nchini. Siku
hii itakuwa inaazimishwa rasmi kila tarehe 12 Disemba.
Mhe Mwenyekiti, Mtetezi wa haki za binadamu ni mtu yeyote, ambaye kama mtu binafsi au kwa kushirikiana na wengine
amejitolea kupigania na kulinda haki za binadamu. Kuwa mtetezi wa haki za Binadamu huhitaji kuwa na shahada wala
stashahada kama alivyopata kusema Jaji Mkuu wa Tanzania Othman Chande. Kazi
hii ni ya kujitolea, kujituma na wakati mwingine kuweka maisha hatarini kwa
ajili ya kutetea wengine. Watetezi wengi hapa nchini wanafanya kazi zao wengi
kwa kujitolea, lakini mwisho wake wengi wameitwa wachochezi ama wapinzani.
Watetezi wa haki za binadamu
wanatambulishwa na kazi zao na mazingira wanayofanyia kazi ili mradi wanafanya
shughuli zao kwa njia ya amani, kwa kuzingatia sheria na miktaba ya kimataifa
ninayowalinda hususani Tamko la Umoja wa Mataifa la Mwaka 1998 Kuhusu Watetezi
wa Haki za Binadamu.
Mhe Mwenyekiti, Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia watetezi
wakikutana na changamoto mbali mbali. Watetezi wamekuwa mara nyingi wakibambikiziwa
kesi mbalimbali, wakipewa majina mabaya kama
vile wachochezi au wapinzani, wamekuwa wakitishiwa na wengine kupoteza maisha.
Kwa hiyo mkutano huu unamaanisha kwamba mawazo ya aina mbali mbali yatawekwa
kwa pamoja kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili watetezi
nchini Tanzania.
Lengo la Siku ya Watetezi
·
Lengo kuu la siku ya watetezi hapa nchini ni
kuwaweka pamoja watetezi wa haki za binadamu, viongozi kutoka serikalini,
washirika katika maendeleo, na washiriki wengineo kutoka sehemu mbali mbali
duniani katika eneo hili la haki za binadamu kwa lengo la kujadili kwa kina
usalama na maslahi ya watetezi wa haki za Binadamu Tanzania.
·
Siku hii pia itakuwa siku maalum ya kuwatunikia
tuzo mbalimbali watetezi wa haki za binadamu, hasa wale waliopata misuko suko
mingi wanapokuwa katika kazi za utetezi.
·
Kualikwa kwa wageni mbalimbali kwenye maazimisho
ya siku hii, hasa wenye uzoefu katika masuala ya haki za watetezi kutaleta fursa
ya kujifunza, na kuangalia namna bora ya kupata ufumbuzi wa changamoto
zinazowakabili watetezi wa Tanzania.
Na pia itakuwa nafasi nyingine ya kuangalia jinsi ambavyo tunaweza kuchota
weledi na uzoefu wa wenzetu wa Ulaya na maeneo mengine.
·
Pia Lengo lingine ni
kuwakumbusha watetezi juu ya majukumu yao na pia
kuwaenzi kwa namna mbali mbali wale ambao wameonesha ujasiri na kusonga mbele
katika kutekeleza majukumu yao
ya kitetezi bila woga pamoja na misukosuko mbali mbali wanayokutana nayo.
·
Siku hii itakuwa siku
maalum kwa watetezi kuonyesha kazi zao, kukutana na wadau mbalimbali, kukaa
meza moja na serikali na kujadili umuhimu wa watetezi wa haki za binadamu na
mashirika yao
katika kuzisimamia haki za binadamu nchini.
Mhe Mwenyekiti, Kwa kuwa leo ni siku ya uzinduzi tu, hatutakuwa na
mambo mengi ya kufanya ila Mtandao utatoa tuzo 2 kwa watetezi wa haki za
binadamu. Tuzo ya kwanza itakwenda kwa Mtetezi wa Haki za Wanawake na Tuzo ya
pili itakwenda kwa kwa Mtetezi Bora wa haki za binadamu vijijini. Watu hawa
wameteuliwa na mtandao kutokana na kazi zao za utetezi wa haki za wengine.
Washindi wa Tuzo hizi wametokana na mapendekezo ya watu waliofanya nao kazi
pamoja lakini pia kutokana na utafiti wa mahitaji ya kiusalama kwa watetezi yalifanyika
katika mikoa 16 na kuhoji watu 330 katika mashirika 200. Wasifu wa kila mshindi
utasomwa baada ya kutangazwa washindi.
Mhe Mwenyekiti, Tunaomba Tume yako iendelee kushirikiana na Mtandao
katika kuboresha usalama wa watetezi hapa nchini na maazimisho ya siku hii ya
watetezi hapa nchini. Pi tunaomba ofisi yako ingilie kati kifungo cha Mtetezi
Bruno Mwambene huko Mbeya.
Hatimaye nawashukuru wote mliohudhuria
uzinduzi huu na Mtandao unaomba mzidi kufikiria zaidi siku hii muhimu kwa
watetezi hapa nchini.
Na Onesmo Olengurumwa
Mratibu Wa Kitaifa Wa
Mtandao
No comments:
Post a Comment