Tuesday, December 24, 2013

Serikali Mkoani Mara kupambana na Changamoto za Wajasiriamali


MUSOMA
 
Serikali mkoani Mara imesema itaendelea kusimamia sera na utaratibu uliowekwa katika kupambana na Changamoto zinazowakabili Wajasiriamali mkoani humo.
 
Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John Gabriel Tuppa katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa wilaya ya Musoma Bw Jackson Msome katika Kongamano la wajasiriamali lililoandaliwa na taasisi isiyo ya Kiseriakli ya Nyangoto Development Group lililofanyika katika ukumbi wa Magereza manispaa ya Musoma mkoani Mara.
                     Bw Jackson Msome   kushoto na Bi Ghati Wassira kulia
Katika hotuba hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mara alisema  kuwa kumekuwepo na Changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wajasiriamali mkoani hapa ambapo serikali ya mkoa itaendelea kusimamia sera na utaratibu ulioweka katika kupambana na changamoto hizo.
 
 "Kama Serikali tunafahamu kuna changamoto nyingi sana ambazo zinawakabili wajasiriamali na kupitia nafasi hii tunasema kuwa tutasimamia Sera na utaratibu uliowekwa ili kusaidia kutatua changamoto hizo" alisema Mkuu huyo wa wilaya
 
Katika hatua nyingine Mkuu wa mkoa wa Mara amewataka wajasiriamali hao kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii CHF  kama njia ya kuimarisha afya zao na familia zao.
 
Kwa upande wake Katibu wa taasisi ya Nyangoto Development Group ambaye pia ni Mjumbe wa baraza la UWT Taifa kutoka mkoani Mara Bi Agness Methew amesema lengo la kuwakutanisha wajasiriamali hao ni kutaka kutambua changamoto zinazowakabili na kutazama jinsi ya kuzitatua kwa kushirikiana na Serikali mkoani hapa.
                                         Bi Agnes Methew
"Kukutana hapa sisi wajasiriamali ni katika kukumbushana na kuangalia Changamoto mbalimbali ambazo zimetukabili kwa Mwaka mzima lengo likiwa ni kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo" alisema Bi Agness Methew
 
Katika hatua nyingne Diwani wa Viti Maalum kutoka wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam Bi Ghati Wassira aliwataka Wajasiriamali hao kushirikiana na Serikali kutatua Changamoto zilizopo ili kuhakikisha wanapiga hatua huku akiiomba serikali kuwasaidia Wajasiriamali hao.
                                        Baadhi ya umati wa Wajasiriamali waliojitokeza
 
Katika Kongamano hilo zaidi ya Wajasiriamali 1000 wanaojihusisha na biashara tofauti walijitokeza ambapo kiasi cha Shilingi milioni kumi na sita zilipatikana katika harambee iliyofanyika katika Kongamano hilo.

No comments:

Post a Comment