Friday, March 29, 2013

MUNGAI AIPONDA KAMATI YA PINDA, ASEMA HAINA JIPYA


aliyekuwa waziri wa elimu na utamadubi mwaka 2000 hadi 2001 Joseph Mungi, akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) juu ya mustakabari wa elimu nchini.
HATIMAYE  waziri wa zamani wa elimu na utamaduni Joseph Mungai, ameiponda kamati  ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza matokeo mabaya ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012  ambayo yaleta historia mbaya kwa Taifa. 
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Iringa, Mungai aliyeiongoza Wizara ya Elimu na utamaduni wakati wa serikali ya awamu ya tatu mwaka 2000-2005, sambamba na kuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini, alisema inafaa matokeo ya mitihani yawe yanatangazwa kwa uwazi hata kama ni mabaya tofauti na ilivyo sasa.
Aidha katika barua yake ya wazi ya Machi 29 mwaka huu yenye kumbukumbu namba JJM/2013/ELIMU/19 iliyoandikwa kwenda kwa Mwenyekiti wa Tume ya Elimu iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuchunguza kufeli kwa  wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012, Mungai ameitaka tume hiyo irejee utafiti uliofanywa na Wizara ya Elimu na Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mwaka 2010 ambayo ilifanya utafiti kudadidi sababu za ufaulu mbaya ambayo pia serikali kushindwa kuusoma utafiti huo bungeni ikihofia madudu yaliyogunduliwa.
Katika barua hiyo, Mungai amehoji sababu za kutoweka bayana ukweli licha ya taarifa hiyo ya utafiti  kuwapo kwenye maktaba za Wizara na kwamba anayoyasema hivi sasa ameyapata kutoka taarifa moja isiyo ya siri ndani ya Wizara ya Elimu.
Ametaka kamati hiyo kutotumia muda na fedha nyingi katika shughuli hiyo ya utafiti ambao majibu yake yapo katika utafiti uliofanywa na kugundua mapungufu ambayo yalifichwa.
Mungai ameitaka tume hiyo ieleze wazi wazi kwamba Taasisi ya Elimu (TIE), iachiwe masuala ya  kutekeleza wajibu wake wa kisheria chini ya sheria ya elimu ya mwaka 1995 ya kuandaa na kuboresha mitaala.
“Tume ya Waziri Mkuu (Pinda) ifanye kwanza rejea ya maandiko ya Wizara ya Elimu ambayo ni Nyaraka za Elimu za mwaka 1999 hadi 2005 na Sheria ndogo za Elimu au kanuni za elimu zilizotungwa kuyapa maboresho hayo uzito wa kisheria yamepelekwa nyaraka za kale kabla ya wakati wake…Hii itasaidia badala ya kutumia muda mwingi na fedha nyingi kugundua upya gurudumu,” inasema sehemu ya barua hiyo ya wazi kwenda kwa Tume ya Waziri Mkuu.
Hata hivyo akijibu maswali ya wanahabari juu ya kukinzana kwa mitaala, kama ipo ua laa, Mungai alisema mitaala ipo ila tatizo ni namna inavyotumika, huku akimkejeri Mbunge wa kuteuliwa na Rais, James Mbatia kuhusu kauli yake aliyoitoa Bungeni miezi michache iliyopita kwamba nchi inaongozwa bila mitaala ya elimu.
Amesema kauli ya Mbatia haikuwa na ukweli kwa vile mitaala hiyo ipo isipokuwa kuna ‘madudu’ katika taasisi za umma zinazohusina na elimu.
Pia amesema Mbatia aliitoa kauli yake bungeni pasipo kufanya utafiti wa kina na kwamba hata wapinzani wa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wanajua kwamba wanasiasa huamua bila kuzingatia ipasavyo utafiti na ushauri wa kitaaluma kuhusu elimu ya taifa letu.
“Kwa hiyo mimi ninaimbia tume ya Waziri Mkuu kwamba utaratibu sahihi wa kupanda madarasa kwa kufaulu uliowekwa na Waraka wa Elimu namba moja na namba mbili wa mwaka 2002 urejeshwe na uimarishwebila kuchelewa ambayo mwalimu mkuu siku zote anayo madaraka ya kukaririsha kama mwanafunzi hajazijua zile ‘K’ 3 yaani kusoma,kuandika na kuhesabu,”Alisema Mungai.
Hata hivyo amewataka wanasiasa kuacha tabia ya kuingilia masuala yenye maslahi kwa Umma hasa elimu, pasipo kufanya utafiti kwa kuwashirikisha wataalamu waliobobea katika masuala y elimu.
Amesema pia michezo mashuleni inachangia kwa kiwango kikubwa kudumaza kama siyo kudidimiza elimu nchini, na kuwa ndiyo sababu kubwa ya yeye kuindoa Umishutamta na umiseta katika awamu yake, kwa madai kuwa wanafunzi na walimu walilazimika kutumia zaidi ya siku 70 katika michezo na hivyoi wanafunzi kupoteza vipindi (Syllabus) .
Ameitaka wizara kuendeleza michezo pasipo kuathiri vipindi vya wanafunzi darasani, kwa kufanya michezo wakati na baada ya masomo, ili kutoathiri taaluma ya elimu.
Amesema kuna haja wadau wanaotoa maoni yao wakasikilizwa pasipo viongozi kuwa na dhana potofu juu ya ushauri unaotolewa na wadau wa elimu, kwani hatua hiyo ni utekerezaji wa ombi la waziri mkuu la kuwataka wadau wa elimu kutoa maoni yao ili kuchangia uboreshaji wa sekta hiyo nyeti.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment