Thursday, January 24, 2013

BODI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA MARA YAZINDULIWA BAADA YA KUTEULIWA NA WAZIRI WA AFYA


WAUUGUZI WA HOSPITALI

Na Shomari Binda
         Musoma

MKUU wa Mkoa wa Mara John Tuppa  aliwataka Wajumbe  wateule wa Bodi ya Hospitali ya Mkoa huo  kufanya mabadliko  katika Hospitali hiyo kwa  kuweka  miundombinu ,wataalam,vitendea kazi,uongozi na usimamizi wa kutosha ili kuiwezesha kutoa huduma za afya zinazokidhi kiwango cha hospitali ya Rufaaa ya Mkoa.

Kauli hiyo aliitoa wakati akizundua  bodi ya hospitali hiyo katika ukumbi wa uwekezaj uliopo katika  ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambayo hivi karibuni ilitangazwa na Waziri wa Afya Dk,Hussen Mwinyi.

Alisema endapo bodi hiyo itasimamia kikamilifu shughuli zake  kutakuwepo  na mabadiliko ambayo ni ya faraja na uchangamfu kwa wananchi kutokana na umuhimu wake wa kutoa huduma iliyo bora  na kutibu magonjwa yaliyoshindikana.

Mkuu huyo aliwahasa wajumbe hao   kujiepusha  na migongano isiyo ya lazima na kutoingilia shughuli za madaktari bali wafanye kazi yao  kwa kufuata maadili mema katika kuboresha huduma  ili hospitali hiyo iweze kufikia kiwango cha rufaa katika kuimarisha utendaji kazi wa watumishi ili kuleta tija .

“Kuimarisha utendaji kazi wa watumishi  ili kuleta tija na kuwepo usimamizi kutoka uongozi wa juu ,kwa kuangalia maslahi yao, na motisha kutafanya kuvutiwa na kupenda  kuendelea kubaki kufanya kazi hapa.

“Nikiwa kama Mkuu na mlezi wa bodi hii ya Mkoa huu wa Mara  naihidi kusimamia nakutoa ushirikiano kikamilifu katika chombo hiki na kiweze kuwa chombo rafiki cha kufanya nacho kazi.”,alisema Tuppa.

Akizungumzia ujenzi wa hospitali ya kwangwa alisema mkoa huo tayari  umeisha patiwa  fedha kiasi cha shilingi bilioni 2 kwa kipindi cha fedha cha mwaka 2012/13 ambapo shilingi bilioni 1.5 zimeishaingia katika mfuko   wa hospitali na kwamba hadi kukamilika  utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 38 ambapo mradi huo utajengwa na shirika la Mfuko wa jamii (NSSF) ili  uendelee kwa haraka zaidi.

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Askofu  wa dayosisi ya kati Kanisa la Mennonite Amos Muhagachi    alisema wapo tayari kujitolea   katika kusimamia  utendaji  kazi ili kuleta tija katika kuendeleza ujenzi wa hospitali  hiyo  ya Rufaa ya mkoa.

"Tumepewa dhamana kubwa ya kusimamia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara kwa kipindi cha miaka mitatu naamini kwa nguvu za Mungu tutashirikiana na wajumbe wengine wa bodi hii ili kufikia malengo,"alisema Askofu Muhagachi

Kwa upande wake Msitahiki Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurula aliipongeza Wizara ya Afya kwa uteuzi huo na kwamba uanzishwaji  wa bodi  ni mzuri kwani utaratibu shughuli za hospitali hiyo ili kupunguza matatizo  ya Wananchi.

“Hospitali kwa kupitia bodi kutaweza kufanikisha shughuli zake kwani bila bodi kunaweza kujisahau na kwenda nje lakini ndani ya bodi hii huwezi kufanya ubadhilifu,”alisema Kisurura.

Hivi karibuni wagonjwa na wauguzi wamekuwa wakilazimika kununua vyombo kama madishi na majagi kwaajili ya kuhifadhi mkojo  wa waguzi wa wagonjwa hasa nyakati za usiku jambo ambalo walisema linaweza kusababisha milipuko mikubwa  ya magonjwa kutokana na baadhi ya wodi katika hospitali hiyo kukosa vyoo.

No comments:

Post a Comment