Mwenyekiti wa Mara Press Club Bw. Emanuel Bwimbo akitoa ufafanuzi juu ya Kongamano hilo
Shomm B akiwa na Mwenyekiti wa Mara Forum Bw George Chibasa
Afisa Program Mwandamizi kutoka MCT Bw Astelius Banzi akitoa neno katika Kongamano hilo
Ahmed Makongo wa Star Tv akiwa mzigoni
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mara Kamishina msaidizi Mwandamizi wa jeshi la Polisi Abslom Mwakyoma akifafanua jambo katika Kongamano hilo na kupelekea mvutano uliokuwepo na Waandishi wa habari mkoani Mara Kumalizika
Mdau nikifafanua Jambo katika Kongamano hilo
Afisa utamaduni Manispaa Mwl Luhende akifafanua Jambo
Mgeni Rasmi katibu tawala mkoani Mara Bw Clement Lujaji
Waandishi wa Habari Mkoani Mara wameamua kumaliza tofati zao na
Jeshi la Polisi baada ya kuweka mgomo wa kuandika Habari kutoka katika Jeshi
hilo tangu Septemba 11 Mwaka huu baada ya kuzuia maandamano ya kupinga kifo cha
mwana habari Daudi Mwangosi.
Maamuzi ya Kusitisha mgomo huo umetolewa leo kwa kauli moja na
Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani humo katika mkutano na wadau wa Habari
uliofanyika katika ukumbi wa uwekezaji wa Mkoa wa Mara.
Kamanda wa polisi mkoani Mara kamishina mwandamizi wa
jeshi la polisi Abslom Mwakyoma kupitia mkutano huo amewaomba radhi waandishi
wa Habari kwa tofauti zilizojitokeza na kusema kuwa Jeshi hilo linawategemea
sana waandishi wa Habari katika kufikisha tofaoti mbalimbali katika jamii.
Alisema kama ni adhabu waliyotoa Waandishi wa Habari kwa
Jeshi la Polisi tangu Septemba 11 wamejifunza na kudai kuwa watahakikisha
tofauti zilizokuwepo zinamalizika na kufanya kazi kama timu katika kuisaidia
jamii.
Amesema hivi sasa kumeibuka makundi ya wahalifu ya Mbio za
vijiti,Mdomo wa furu,Jamaica mocas na G5 ambayo yametishia amani kwa wananchi
wa Manispaa ya Musoma na wakati mwingine kusababisha mauji ya raia, hivyo
alisema jeshi hilo limejipanga kukabiliana na makundi hayo kuanzia sasa na
kueleza bila ushirikiano na Waandishi wa Habari hawawezi kufanikisha.
Kuhusu hatua ya waandishi wa habari mkoani Mara kususia kuandika
habari za jeshi la polisi kutokana na kuzuiwa kwa maandamano hayo,kamanda
Mwakyoma,alisema hatua hiyo ilichukuliwa baada ya kubaini kuwa maandamano hayo
hayakufuata taratibu za sheria.
Awali katibu tawala mkoa wa Mara Bw Clement Lujaji,akizungumza
wakati akifungua mkutano huo,amewaomba waandishi wa habari mkoani Mara kufanya
kazi kwa kuzingatia uzalendo pamoja na kuibua fursa zitakazo lenga kuchochea
ukuaji wa uchumi wa wananchi wa mkoa wa Mara.
Alitumia nafasi hiyo,kuliomba jeshi la polisi na waandishi wa
habari mkoani Mara,kuondoa tofauti zao ambazo zilijitokeza na kusababisha
kususiwa kuandikwa kwa habari za jeshi hilo na hivyo kuwanyima haki wananchi
kupata habari ambao ni haki yao ya msingi.
Kwa sababu hiyo waandishi wa habari wa mkoa wa Mara kwa kauli moja
chini ya uenyekiti wake Bw Emanuel Bwimbo,walitangaza kuondoa mgomo wa kuandika
habari za jeshi la polisi kuanzia sasa na kwamba wamemtaka kamanda wa polisi
kukemea unyanyasaji ambao umekuwa ukifanywa na askari wake dhidi ya waandishi
mkoani Mara.
No comments:
Post a Comment