Thursday, August 16, 2012

           WAKAZI WA MARA WASHAULIWA KUACHANA NA  TABIA AMBUKIZI
Na Emmanuel Chibasa, Musoma

WANANCHI Mkoani Mara wameshauliwa kuacha tabia ambazo zimekuwa zikichangia kasi kubwa ya kuongezeko la maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi.

Wito huo umetolewa jana mjini Musoma na Mratibu wa kitengo cha kuhudumia watu wanaishi na virusi vya Ukimwi CTC katika hospitali ya mkoa wa Mara Bi Hellen Kure,wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake.
Waandishi wa habari wa mkoa wa Mara waliokuwa kwenye mafunzo ya uandishi wa habari za afya wakiwa ofisi ya mganga mkuu wa mkoa kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali za afya mkoani humo,mafunzo hayo siku nne yameendeshwa chini ya muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania(UTPC)yanalenga kuwajengea uwezo waandishi kuandika habari za afya kwa usahihi
Mratibu huyo wa CTC katika hospitali ya mkoa wa Mara, alitoa taarifa hiyo juu ya huduma zinazotolewa na kituo hicho kwa waandishi hao ambao wako katika katika mafunzo ya uandishi wa habari za afya chini ya ufadhili wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari nchini UTPC inayofanyika katika ukumbi wa orange tree musoma.

Akielezea juu ya hali halisi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi tangu kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 2004 mpaka sasa, alisema idadi ya wagonjwa imekuwa ikiongezeka kila kukicha huku kundi la vijana likiongaza.

Alizitaja sababu kubwa zinazochangia maambukizi ya ukimwi ni pamoja na kufanya ngono zembe, wazazi wa kiume kuwa mbali na familia kwa muda mrefu kwa shughuli za kikazi zikiwemo za uvuvi na uchimbaji wa madini jambo linalowafanya kujingiza mapenzi mapya.

Hata hivyo Bi Kure,aliesema kuwa kituo hicho kinapokea idadi kubwa ya watu ambao wamekuwa wakijitokeza kwajili ya kupima hasa kutoka sehemu mbali mbali za wilaya za Mkoa wa Mara,huku wengi wao wakiogopa kupima katika vituo viliopo maeneo jirani na wanapoishi kwa kuogopa kunyanyapaliwa .

Kwa sababu hiyo alisema hali hiyo imesababisha msongamano wa Wagonjwa katika kituo hicho,huku akitoa wito kwa Wagonjwa kuacha tabia ya kujinyanyapaa wenyewe hivyo waendelee kutumia vituo viliopo katika maeneo yao.

“Wakati mwingine pia baadhi ya tabia za watoa huduma za kutoa siri za wagonjwa zimekuwa zikisababisha wagonjwa kuogopa kupata matibabu katika maeneo wanayotoka ingawa jambo hili si kubwa sana’alisema mratibu huyo CTC.

Takwimu za kituo hicho cha hospitali ya mkoa zimeonesha kuwa kuanzia mwaka October mwaka
2004 hadi mwaka 2011 kati ya watu waliojitokeza kupima 43,800 sawa na asilimia 7.0 walikutwa na maambukizi ya ukimwi na kuanza kutumia dawa za kuvubaza virusi vya ukimwi.

Kwa mujibu taarifa hizo katika kituo hicho tu watu 148 wameripotiwa kufariki dunia wanawake 77,wanaume 66,watoto wakike 2 na watoto wakiume 3 ingawa idadi ya vifo inaweza kuongeka kutokana na ndugu kutotoa taarifa baada ya vifo kutokea kuhusiana na ukimwi.

Kuhusu changamoto zinazokikabili kituo hicho alisema ni pamoja na kubadilishwa mara kwa mara kwa watoa huduma hali inayowaathilipia wagonjwa na utendaji kazi wa kituo kutokana na mazoea.

“Wanapobadilisha watoa huduma mara nyingi imechangia wagonjwa kukimbia huduma hata wakati mwingine kushindwa kuendelea na tiba”aliongeza.

Alitaja changamoto nyingine zinazokikabili kituo hicho ni pamoja na watoa huduma kubadiliswa wakati wakiwa tayari wamepata mafunzo maalumu kwajili ya kuwahudumia wagonjwa hao,kukosekana kwa gharama za mawasiliano kwajili ya kuwakumbusha wagonjwa kuhusu matumizi ya dawa pamoja na usafiri kwajili ya wahudumu ili kuwatembelea wagonjwa majumbani.

Kuhusu sababu zinazochangia wagojwa kukatisha matibabu ni pamoja na kukosa nauli kwajili ya kufata dawa`katika kituo kwa wale waliombali zaidi jambo linalopelekea wakati mwingine kuacha kutumia dawa kwa muda muafaka na hivyo kusababisha usugu na kuhatarisha maisha yao.

No comments:

Post a Comment