Wednesday, July 25, 2012

               MAADHIMISHO   YA  MASHUJAA  MKOANI  MARA

                      Mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tuppa akisoma taarifa ya serikali
          Mkuu wa Mkoa akisalimiana na Baadhi ya wageni katika Maadhimisho hayo
  Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mara Kamishina Mwandamizi wa jeshi la Polisi Abslom Mwakyoma
 Mkuu wa mkoa wa Mara akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Polisi mkoani Mara
             Furaha pale watu wanapokutana na kukumbushana mambo ya nyuma
                                  Mnara uliowekwa katika eneo ambalo ndege ilianguka
Wapambanaji wakiwa katika eneo la kumbukumbu ya mashujaa


Maadhimisho ya siku ya Mashujaa mkoani Mara yamefanyika leo katika Viwanja vya  Kanisa la RC Rwamlimi huku mgeni rasmi akiwa mkuu wa mkoa wa Mara Bw. John Tuppa.

Katika Madhimisho hayo  Mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tuppa amesema  kuwa ipo changamoto  kubwa kwa viongozi wa Manispaa ya musoma,wadau na viongozi mbalimbali kuwaenzi Mashujaa waliosaidia kuikomboa nchi Tanzania.

Amesema ni vyema wananchi wa mkoa wa Mara kuendelea kufuata nyayo za Mashujaa wetu,kulinda hazina za Ujasiri,Uzalendo,Umoja na Mshikamamo walizotuachia. 

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mara amesema kuwa watanzania wasiichee Amani tuliyonayo kwani haikujengwa siku moja na kama tutathubutu kuiacha itaondoka Mara moja lakini itatugharimu muda mwingi na jasho jingi kuirudisha.

Amesema ni vyema wananchi wakashiriki  vizuri katika Zoezi la Sensa litakaloanza August 26,2012 na pia kuhudhuria kwa wingi ili kutoa maoni yao kwa furaha na Amani pale tume ya kupokea maoni juu ya katiba mpya itakapopita kwenye maeneo huska.

Mkuu wa mkoa Tuppa amesema maadhimisho hayo yataendelea kuboreshwa kwa miaka inayokuja ikiwa ni njia sahihi ya kuwaenzi Mashujaa walioikomboa Tanzania

No comments:

Post a Comment