Thursday, April 26, 2012

SERENGETI
Mwanaume mmoja wa wilaya ya Tarime mkoani Mara,anadaiwa kuitelekeza familia yake yenye watoto wanne walemavu aliowazaa na mke wake wa ndoa kwa madai
ya kukwepa mkosi, jambo ambalo limemlazimu mwanamke huyo kuishi maisha ya kutegemea misaada ya majirani kwa ajili ya mahitaji ya watoto wake.

Bi Esther Chacha mkazi wa kitongoji cha Songambele kata ya Sabasaba wilayani Tarime,amesema baada ya kuzaa watoto watano, wanne wakiwa ni walemavu, mme wake huyo ambaye amemtaja kwa jina la Chacha Merengo,aliikimbia familia hiyo na kuoa mke mwingine kisha kwenda kuishi mjini Mugumu Wilayani Serengeti,kwa madai kuwa hawezi kutunza watoto wasio na faida.

Aidha mama huyo ameiomba Serikali na wasamalia wema, kumsadia kutunza watoto hao wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kumsomesha mtoto mmoja ambaye amebahatika kuzaliwa bila ya kuwa na ulemavu katika familia hiyo,ambaye kwa sasa anasoma darasa la saba katika shule ya msingi ya Mturu katika kata ya Rebu ambayo imekuwa akihitunza tangu mwaka 2005 alipachwa na mme wake

Nao baadhi ya majirani wa mama huyo,Bi Esther Eliah na Bi Rose Yohana,wameomba watu ambao wataguswa na mateso anayopata mama huyo katika kulea watoto hao kutoa msaada ambao utamuwezesha kuwatunza watoto wake.

Hata hivyo mme wa mama huyo Bw Chacha Merengo,alipotafutwa kwa njia ya simu kwa zaidi ya mara nane ili kuthibitisha madai hayo hakuweza kupatikana kutoka na simu yake ya mkononi muda wote kuwa imezimwa na juhudi za kumtafuta bado zinaendelea.

No comments:

Post a Comment