Sunday, April 29, 2012

Mripuko kwenye kanisa mjini Nairobi, Kenya, umeuwa mtu mmoja na kujeruhi wengine kadha.

 Polisi wanasema mripuko huo katika kanisa la God's House of Miracle kwenye mtaa wa Ngara, ulisababishwa na guruneti.

 Kumetokea mashambulio kadha ya maguruneti nchini Kenya tangu mwaka jana pale serikali ilipotuma wanajeshi Somalia kupambana na wapiganaji wa Kiislamu, Al-Shabaab.


No comments:

Post a Comment