wananchi wenye hasira kali wa kijiji cha saragana musoma vijijini waliokuwa doria wamemuua mwita maseke kwa kutumia silaha za jadi baada ya kukutwa akiswaga ngombe saba aliowaiba katika kijiji cha buramba wilayani bunda mkoani mara
akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kaimu kamishna wa polisi mkoani mara acp robert boaz amesema uchunguzi umeonyesha kuwa marehemu aliiba ngombe hao katika kijiji cha bulamba na amemtaja mmiliki wa ngombe hao kuwa ni kasheki lusona
kamanda amesema kuwa katika tukio hilo marehemu hakuwa peke yake bali alikuwa na watu wengine wawili waliofanikiwa kukimbia na haijulikani ni wapi walipoelekea lakini jeshi la polisi bado linafanya uchunguzi ili kuwabaini watuhumiw hao
kamanda amewataka wananchi kutojichukulia sheria mikononi wafuate utaratibu kwani wanapofanya hivyo wanapoteza ushahidi na kwamba wanapowakamata wahalifu wawapeleke katika vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua
,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Rorya
madiwani wa halimashauri ya wilaya ya rorya mkoani mara wamewataka wataalamu wa halimashauri cmt kuwapa majibu sahihi katika kikao cha baraza lijalo juu ya matumizi ya shilingi milioni 51 zilizotumika kujenga barabara ya kilomita 2 kwa madai kuwa pesa iliyotumika ni kiasi kikubwa hakiendani na utengenezaji
wakiongea katika kikao cha cha baraza la madiwani madiwani hao wameomba ufafanuzi na mchanganuo wa fedha kutoka kwa wataalamu juu ya kiasi hicho cha fedha lilichotumika kwa madai kuwa kiwango kilichopitishwa cha utengenezaji wa barabara hiyo inayotoka makao makuu ya wilaya ingri juu hadi saro kilikuwa ni shilingi milioni 35 lakini badala yake pesa hizo ziliongezeka na kufikia sh.milioni 51.
aidha diwani pita ayoyi wa kata ya mirare ambaye pia alikuwa diwani miaka 5 liyopita amesema kuwa anashangazwa na cmt kuongeza kiasi cha sh. million 16 ambapo wakati wana vunja baraza kiwango kilichopitishwa kwa uhalari cha utengenezaji wa barabara kilikuwa sh milioni 35.
kwa upande wake kaimu mhandisi wa ujenzi julius kahena aliwajibu madiwani hao kuwa barabara haikuwa kwenye bajeti na haukuwepo mpango kazi hivyo kiwango cha milioni 35 kisingetosha barabara ya km 2 kwa sababu hapakuwa na barabara.
hata hivyo madiwani hawakulizishwa na majibu hayo ya mhandisi na hivyo kumwagiza yeye pamoja na wataalamu wa (cmt)kufanya upya mchanganuo na kupima upya ili madiwani hao wajilizishe kilichoongezeka na namna fedha zilivyotumika.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Tarime
mkurugenzi wa halimashauri ya wilaya ya tarime mkoani mara fidelis lumato amesema hana kesi na mtendaji wa kata ya matongo deodatus weikama aliyekamatwa na polisi hivi karibuni kwa agizo la mkuu wa wilaya ya tarime john henjewele.
lumato amesema kuwa yeye hausiki na kukamatwa kwa mtendaji huyo na kuongeza kuwa endapo akibainika kutofika kazini kwa mtendaji huyo kwa muda wa wiki mbili atachukuliwa hatua za kinidhamu
awali kukamatwa kwa mtendaji weikama kumekuja baada ya mkuu wa wilaya john henjewele kudai kuwa ofisi yake imepata malalamiko ya bi nchagwa kisire (36) kuporwa ardhi na mme wake kisha kushirikiana na mtendaji huyo kufunga nyumba yake januari 23,huku akisababisha mwanae na watoto 3 kuhifadhiwa na majirani
aidha kwa upande wake mtendaji wa kata ya matongo deodatus waikama alipohojiwa na mwandishi wa habari hii mjini tarime baada ya kuachiwa huru na polisi amesema kuwa yeye hakuhusika kufunga nyumba ya bi nchagwa kisire anayelalamika kuporwa kwa ardhi yake na mme wake ambapo pia alilionyesha vielelezo mbalimbali kuhusiana na malalamiko ya mama huyo.
mtendaji huyo amepinga kauli ya dc ya yeye kushindwa kutatua migogoro ya wananchi hususani malalamiko ya kisire ya uporwaji ardhi ambapo amesema kuwa tayari alikuwa ameshawaita yeye na mme wake ofisini kusuluhisha mgogoro huo baada ya malalamiko hayo kuyapata kutoka ofisi ya kijiji cha nyangoto.
mbali na hivyo pia amesema lalamiko hilo alilifikishwa katika baraza la ardhi na nyumba wilayani tarime baada ya mmewe kukataa kusuluhushwa kwa kile alichoeleza kuwa yeye ndiye kichwa cha nyumba lazima asikilizwe.
mkuu wa wilaya john henjewele alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya kumuhoji mtendaji weikama baada ya kuachiwa huru alisema kuwa mwandishi huyo ataipata taarifa ofisin kwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo .
kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi tarime/rorya jastus kamugisha alipohojiwa juu ya upelelezi unavyoendelea dhidi ya mtendaji huyo kamanda huyo alisema kuwa polisi haiusiki kwani walitekeleza agizo kutoka kwa dc.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
No comments:
Post a Comment