Monday, July 4, 2011

TUTAFAKARI KABLA YA KUFANYA MAAMUZI

Nimesia kuwa baadhi ya wananfunzi katika chuo kikuu cha Dodoma UDOM watafukuzwa chuo kutokana na kuhusika na mgomo chuoni hapo,ni kweli si sahihi kuweka mgomo katika vyuo vyetu hasa ikizingatiwa serikali inatumia fedaha nyingi katika kugharamia wananfunzi hao.

Lakini pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali kusema kuwa watatafuta vinara wa migomo ili kuwafuza chuo sidhani kama ni sahihi maana jambo ambalo lilitakiwa kwasasa ni kutafuta chanzo cha mgomo na si kuwafukuza wanafunzi hao bila kutafuta chanzo cha mgomo huo maana ninavyoelewa mgomo huo tena utarudia kama hawatakuwa wametibu au wamepata chanzo hicho.

Kauli yangu kwa viongozi wetu ni kwamba wasitumie nguvu ya madaraka waliyonayo katika kukandamiza watu wengine wasiokuwa na madaraka,tuachanae na hisisa kuwa pengine viongozi wa vyama vyama vya upinzani ndio wanachochea migomo kwenye vyuo vyetu mbona wakati wa Baba wa Taifa migomo ilikuwepo ina maana wapinzani ndiyom walikuwa chanzo? Viongozi wetu msikwepe majukumu yenu kwa kuweka visingizio

Na Mwana wa Afrika

No comments:

Post a Comment