Na Mohammed Mhina, Handeni
HANDENI IJUMAA SEPTEMBA 14, 2012.
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mkoani Tanga, Bw. Muhingo Rweyemamu,
amewataka vijana wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo zikiwemo za
matunda, kujiunga katika vikundi na kuanzisha mashamba ya miti ya
matunda badala ya kuwa wakaakati.
Mkuu
huyo wa Wilaya ametoa wito huo wakati akizungumza na Vijana katika
maeneo ya Chanika na Segera mpakani mwa wilaya za Handeni, Korogwe na
Muheza mkoani Tanga.
Bw,
Rweyemamu amesema kama vijana watajiunga katika vikundi na kuanzisha
mashamba ya miti ya matunda wataweza kunufaika kwa kuinua vipato vyao na
kubadilika kimaisha.
Amesema
kazi ya uchuuzi wa matunda kwa kuyatembeza mikononi, hayataweza
kuwakomboa kiuchumi kwa vile faida kubwa itaishia kwa wakulima
wanakochukua matunda hayo tofauti na kama watakuwa na mashamba yao.
Hata
hivyo, Mkuu huyo wa wilaya ya Handeni amesema kama vijana wataungana na
kuanzisha vikundi vya ushirika itakuwa rahisi kwa Serikali kuwapatia
huduma zikiwemo za mikopo ya kukuza mitaji yao.
Amesema
tayari wilaya ya Handeni imenunua matrekta kwa ajili ya kuwalimia watu
mbalimbali wakiwemo vijana wenye vikundi vya ushirika.
Mkuu
huyo wa wilaya ya Handeni amewataka vijana hao kuiga mfano wa vijana
wenzao wa Kijiji cha Misima wilayani humo ambao wamejiunga pamoja na
kuomba kupatiwa eneo la Kilimo kutoka Serikali ya Kijiji.
Katika
ziara hiyo, Bw. Rweyemamu alifuatana na wataalam mbalimbali wakiwemo
Maafisa Ushirika wa wilaya hiyo ambao nao wamekuwa wakitoa elimu za
masuala ya ushirika.
Idadi
kubwa ya Vijana waliopo katika Wilaya ya Hendeni, wamekuwa
wakijishughulisha na masuala ya biashara ndogondogo zikiwemo za matunda
mbali ya kuwepo kwa maeneo makubwa ya kilimo.
No comments:
Post a Comment