Thursday, September 13, 2012

AFISA UHAMIAJI MKOA WA MARA AMTISHIA AFISA WAKE KWA KISU

MUSOMA

AFISA Uhamiaji Mkoa wa Mara  Bw Jacob Sambai anadaiwa kumtishia kwa Kumchoma Kisu Mfanyakazi mmoja wa Idara Hiyo Moses Malekela kwa kile kinachodaiwa bosi huyo kuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti ambaye pia ni mfanyakazi wake.(jina tunalo) 

Taarifa zinasema kuwa Vitisho hivyo vilitokea Agost 24 Mwaka huu majira ya saa nane mchana baada ya bosi huyo kupokea malalamiko kutoka kwa afisa mmoja ndani ya ofisi hiyo Sackibu Kabyemela aliyekuwa akituhumiwa na binti huyo kuwa anatoa taarifa za kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi na bosi huyo

Kufuatia kuwepo kwa Taarifa hizo katika ofisi hiyo ndipo bosi huyo alipoitisha kikao cha dharura kwa kuwahusisha msaidizi wake DCI Milinga, maafisa waliohusika na tuhuma hizo pamoja na maafisa wengine kama mashaidi.

Katika kikao hicho Maafisa hao kila mmoja alijieleza kwa muda wake huku wakisisitiza kuwa hizo ni taarifa ambazo ziko ofisini na kila mtumishi wa ofisi hiyo anajua kuwa bosi anatembea mmoja wa Mfanyakazi katika Idara hiyo

Bosi mimi na mwenzangu tunaotuhumiwa kusambaza uvumi huo hatukuwepo ofisini kwa muda mrefu,tulikuwa masomoni tuliporipoti na sisi tukayakuta hayo maneno. Fanya uchunguzi” Alisikika mtumishi mmoja akisema.

Aidha katika hatua Nyingine Ikafika wakati  wa mtumishi wa mwisho Moses Malekela kujieleza ambapo nae akasema, “Bosi, haya ni maneno tu, fanya uchunguzi wa kina utapata ukweli wake”.

Baada ya Kusikiliza watumishi wote waliokuwepo katika kikao hicho ndipo Bosi huyo akapandisha jazba na kuvuta droo yake na kuchomoa kisu kikali na bisibisi na kutaka kumchoma afisa huyo,ndipo alipozuiwa na msaidizi wake akishirikiana na maafisa wengine waliokuwepo kwenye kikao na kuamua kuweka kisu chini na kuvua saa yake ya mkononi tayari kwa kumpiga ngumi afisa huyo huku akisema,” Leo kazi na iishe”

Tafrani hiyo ilichukua takribani dakika kumi ambapo bosi huyo akitaka kuonyesha umwamba wake lakini busara za msaidizi wake na maafisa waliokuwepo walifanya kazi ya ziada kumzuia bosi huyo na baada ya kuona amezidiwa nguvu ndo akamtolea kauli ya vitisho huku akisema “Haina shida, ntakutafuta mtaani”

Kauli hiyo ilimtisha mtumishi huyo  Moses Malekela na kuamua kutoa taarifa kituo kikuu cha Polisi Musoma kwa RB NO MUS/RB/5872/2012 na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ngazi ya mkoa ili kulinda usalama wa maisha yake.

Akiongea kwa njia ya Simu na Mwandishi wa habari hii Kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi Mwandizi wa Jeshi hilo Abslom Mwakyoma alisema kuwa tayari suala hilo limefika katika hilo na linafanyiwa uchunguzi wa kina kabla ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa

 “ Ni kweli Suala hilo lipo tayari Katika Jeshi letu na tunaendelea kulifanyia uchunguzi wa kina kabla ya hatua zaidi za kisheria hazijachukuliwa” alisema Kamanda huyo

Naye Afisa Uhamiaji huyo alipoulizwa kwa njia ya Simu kuhusu Sakata hilo alisema kuwa tayari limefikishwa kwenye Vyombo vya sheria hivyo ni vyema suala hilo likafanyiwa kwanza Uchunguzi na baadaye tutapata ukweli.

  ‘Hayo unayosema yapo na tayari yapo Polisi hivyo nadhani ni vyema kwanza tukasubiri tuone baada ya Uchunguzi wa jeshi hilo ndipo ukweli utabainika” alisema Afisa Uhamiaji huyo

Wakati huo huo kuna taarifa rasmi kuwa bosi huyo amekuwa na Tabia ya kuwatongoza maafisa wake wa kike na pale wanapomkatalia huwachukulia hatua kwa kuwahamisha vitengo ama kuwatenganisha wanandoa hao kwa kuwahamishia vituo vya mbali.

Tuhuma nyingine zinazomkabili bosi huyo, ni pamoja na kukarabati jengo la ofisi kwa gharama zisizoendana na ukarabati huo, Kufanya manunuzi ya thamani za ofisi bila kufuata taratibu za manunuzi ya umma.

Mbali na hivyo pia inadaiwa Kuendesha gari STK 2559 yeye mwenyewe bila kibali cha katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani na kuliangusha katika maeneo ya Kiabakari bila ya kuwa na dereva wa serikali na kuitengeneza gari hiyo kwa gharama za kodi za walalahoi wa bila kufuata taratibu.

Taarifa  zaidi zinasema kuwa baada ya kuitengeneza kinyemela gari hilo,Bosi huyo aliandika barua TEMESA kwa ajiri ya ukaguzi wa gari hilo na TEMESA wakajibu kukataa kuikagua kwa barua kumbukumbu  NO MUS/STK 2559/249/34 kwa maelezo kuwa haikufuata taratibu za magari ya serikali yanapopata ajali

  “Hayo kwangu siyo Malalamiko mapya ndugu yangu maana yamekuwepo muda mrefu ila wewe kama unataka kuuza gazeti kwa habari hiyo wewe andika.Alisema Afisa huyo

Taarifa zaidi zinasema kuwa Malalamiko hayo yote yalisha tumwa uhamiaji makao makuu na ikawa kimya, na mengine yakatumwa kwa katibu mkuu ambae alituma tume ya mtu mmoja na kufanikiwa kuwahoji watumishi ambapo mpaka sasa bado hatima yake haijajulikana

No comments:

Post a Comment