MUSOMA
CHAMA cha Waandishi wa Habari mkoani Mara MRPC,
kimemfukuza uanachama wa chama hicho, mwandishi wa habari wa radio Free Afrika
mkoani Mara Bw Maxmilian Ngesi baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho
yaliyofikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za jeshi la polisi mkoani humo.
Akizungumzia kufukuzwa kwa Mwandishi huyo mwenyekiti
wa chama hicho Bw Emmanuel Bwimbo,alisema
kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada
ya kusikika akitangaza habari za jeshi la polisi kwa kumkariri kamanda wa
polisi wa mkoa wa Mara.
“ Sisi kwa
kauli moja tumekubaliana kutofanya kazi na Jeshi la Polisi Mkoani Mara baada ya
Matukio kadhaa likiwemo ya kuuawa kwa mwandishi wa habari mkoani Iringa na
kutunyima kibali cha Maandamano yetu ya Amani kupinga Mauaji hayo” alisema Bw
Bwimbo
Bw Bwimbo alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi
gani mwandishi huyo alivyokiuka makubaliano ya pamoja na kuwasaliti wenzake
ambao wamekubaliana kwa pamoja kuwa hawataandika habari za jeshi hilo kutokana
na kuzuiwa waandishi kutoandamana katika maandamano ambayo yaliitishwa nchini
kote kulaani kitendo cha mauaji ya mwandishi wa kituo cha chanel Ten mkoani
Iringa Daud Mwangosi.
Alisema Ngesi kama mwanachama alitakiwa kutii
maamuzi ya chama na tamko la chama chake kwa vile tamko hilo limewataka
wananchama wote na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa
matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kinyume.
Aidha Mwenyekiti huyo alisema kamwe chama hicho
hakiwezi kuvumilia mwandishi atakaye kiuka agizo hilo na hatua ambayo
imechukuliwa kwa Ngesi ni mfano kwa waandishi wengine hadi hapo tamko
hilo litakapo tenguliwa.
Akiongea kwa njia ya Simu na Mtandao huu,Mwandishi huyo alisema kuwa alifanya hivyo bila kuwa na taarifa zozote kama kuna msimamo wa chama katika kufanya kazi na Jeshi la Polisi mkoani Mara.
Bw Maximillian Ngessi alisema kuwa anajuti kwa hilo na uongozi wa Chama hicho cha Waandishi wa Habari Mkoani hapa kimefanya uamuzi huo kwa haki,aidha aliongeza kuwa anajutia kwa hilo kutokana na kutokuwa na taarifa zozote kutoka katika Chama hicho.
"Ni kweli nimevuliwa uanachama lakini ni sahihi maamuzi hayo kwani nimekwenda kinyume na makubaliano ingawa nimetoa taarifa hiyo bila kuwa na taarifa zozote kutoka ofisini na pia najutia kwa hilo" alisema Bw Ngessi
Akiongea kwa njia ya Simu na Mtandao huu,Mwandishi huyo alisema kuwa alifanya hivyo bila kuwa na taarifa zozote kama kuna msimamo wa chama katika kufanya kazi na Jeshi la Polisi mkoani Mara.
Bw Maximillian Ngessi alisema kuwa anajuti kwa hilo na uongozi wa Chama hicho cha Waandishi wa Habari Mkoani hapa kimefanya uamuzi huo kwa haki,aidha aliongeza kuwa anajutia kwa hilo kutokana na kutokuwa na taarifa zozote kutoka katika Chama hicho.
"Ni kweli nimevuliwa uanachama lakini ni sahihi maamuzi hayo kwani nimekwenda kinyume na makubaliano ingawa nimetoa taarifa hiyo bila kuwa na taarifa zozote kutoka ofisini na pia najutia kwa hilo" alisema Bw Ngessi
Jumatatu wiki hii waandishi wa habari walifanya
maandamano nchi nzima wakilaani mauaji ya mwandishi mwenzao Daudi
Mwangosi ambapo kwa mkoa wa Mara maandamano hayo yaliuzuiwa na polisi
hali iliyofanya chama cha waandishi wa habari kukataa kuandika habari za jeshi
hilo mkoani Mara.
No comments:
Post a Comment