DC AFUNGUA MAFUNZO YA SENSA MUSOMA
Pendo Mwakyembe
MUSOMA
Washiriki wa mafunzo ya sensa
ya watu na makazi Waagizwa kufuatilia na kusikiliza kwa makini mafunzo
watakayopewa na wawezeshaji wa zoezi hilo ili kuleta ufanisi katika zoezi hilo.
Hayo yamesemwa na mkuu wa
wilaya ya Musoma Bwana Jackson Msome wakati akifungua semina ya sensa na
makazi
katika ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mara.
Mkuu wa wilaya ya Musoma,Bw Jackson Msome
Bwana Jackson amesema kuwa
mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kupata mbinu za kuuliza maswali, namna ya
kudodosa taarifa mbalimbali za kaya na kujua kutambua namna ya kuhifadhi siri
na taarifa za kaya ambazo wamezipata.
Amesema kamati imewaamini
kufanya kazi hiyo hivyo washiriki wanaombwa watambue dhamana kubwa waliyopewa
na serikali hivyo ufanisi na uhodari wao katika kazi utapimwa kwa mafanikio ya
sensa iyo itakayoanza tarehe 26, mwezi wa nane 2012.
Aidha ameongeza kuwa serikali
inapenda kuona sensa hiyo ikipata mafanikio makubwa hivyo semina hiyo inalenga
kuwajengea uwezo mkubwa na ufanisi ili kila wilaya ifanikishe zoezi hilo kwa
ufanisi zaidi kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.
Wakati huohuo mkuu huyo wa
wilaya ameviomba vyombo vya habari kutoa ushirikiano mkubwa katika kuelimisha
wananchi kuhusiana na sensa ya watu na makazi.
Amesema vyombo vya habari
vina nguvu na mchango mkubwa katika kutoa elimu ya uhamasishaji hivyo ni vema
kama vyombo hivyo vitatumia nafasi hiyo kuhamasisha wananchi ili watoe ushirikano wa kutosha katika zoezi hilo.
Mafunzo hayo ya sensa ya watu
na makazi yamefunguliwa rasmi hii leo katika wilaya ya Musoma na yatadumu kwa siku kumi na moja. Zoezi la
kuhesabu watu na makazi litaanza mwezi huu tarehe ishirini na sita.
No comments:
Post a Comment