Baadhi ya wajumbe wakiwa ndani ya ukumbi wa CCM mkoa wa Mara
Mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tuppa akifungua semina ya wakufunzi wa sensa mkoani Mara
Wajumbe wakiwa katika semina
Wajumbe wakiwa kwenye semina ya sensa
Mkuu wa mkoa wa Mara Bw. John Tuppa akiwa na Mwakilishi wa walemavu katika semina hiyo mjini Musoma leo
Mwana wa Afrika nikiwa na Mdau Shomary wa Binda
George Marato wa ITVVVVVVVVVVVVVVVVVV
Wakuu wa wilaya Mkoani Mara
MUSOMA
SERIKALI
mkoani Mara,imeviagiza vyombo vya dola na viongozi mbalimbali wa ngazi zote mkoani
humo,kuhakikisha wanasimamia hali ya usalama kwa kuwachukulia hatua kali watu wote
ambao wataonekana kukwamisha mafanikio ya zoezi la Sensa ya watu na makazi,ambalo
linatarajia kufanyika nchini kote kuanzia Agosti 26 mwaka huu.
Kauli hiyo
imetolewa mjini Musoma na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia
ni mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Gabiriel Tupa wakati akifungua mafunzo ya wiki
mbili ya wakufunzi wa Sensa ya watu na makazi ngazi ya mkoa.
Alisema
serikali haitakubali baadhi ya watu kuwa chanzo cha kukwamisha zoezi hilo muhimu
kwa taifa na ambalo linatarajia kiasi kikubwa cha fedha,ambapo amesema ni
wajibu wa kila kiongozi kufanya uhamasishaji kwaajili ya kuwezesha mafanikio
katika zoezi hilo.
Hata hivyo
mkuu huyo wa mkoa wa Mara,alitumia nafasi hiyo kuonya kwamba kamwe serikali hatasita
kuchukua hatua kwa wakufunzi hao na kwamba haitakubali kupokea visingizio vya
aina yoyote kutoka kwao baada ya kupata mafunzo hayo.
Kuhusu
wasiwasi wa wananchi wa kupoteza muda wakati wa zoezi hilo,mkuu huyo wa mkoa wa
Mara,alisema zoezi la sense halitaweza kukwamisha shughuli za wananchi kiuchumi
na kwamba watoe taarifa sahihi kwa makarani bila ya hofu kwa vile taarifa hizo mbali na kuwa za siri
pia zitawezesha taifa kupanga mipango yake mbalimbali ya maendeleo.




















No comments:
Post a Comment