RC AWATAKA WATANZANIA
WAISHIO NJE YA NCHI KUWEKEZA NCHINI.
Dinna
Maningo,Tarime
MKUU wa Mkoa
wa Mara John Tuppa amewataka Watanzania waishio nje ya nchi na wale wenye uwezo
wa kipato kusaidia katika Nyanja mbalimbali za maendeleo hususani watoto yatima
na waishio katika mazingira magumu.
RC Tuppa
alisema kuwa endapo watu wenye uwezo watajitokeza kwa wingi katika kusaidia
watoto yatima na wa mazungira magumu
katika kuhakikisha wanapata elimu itasaidia kupunguza tatizo la watoto
wanaolandalanda mitaani.
Mkuu wa mkoa wa Mara Bw.John Tuppa
Hayo
yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mara
Bw.John Tuppa wakati alipotembelea kituo cha kulelea watoto yatima na wale wa
mazingira magumu kinachofahamika kwa jina la CITY OF HOPE kilichopo kijiji ncha
Ntagacha kata ya Genyange Wilayani Tarime kilichoanzishwa na Docta John Chacha
aishie nchini Marekani kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
“Watanzania
wenye uwezo wa kipato wenye elimu na waishio nchini na nje ya nchi wawekeze
hapa nchini ili kusaidia wananchi hususani katika maswala mbalimbali yakiwamo ya
kuhakikisha watoto yatima na wamazingira hatarishi wanapata elimu hii itasaidia
kupunguza umaskini kwani hao watoto watakuwa na elimu itakayowasaidia katika
maisha yao ya baadae badala ya kuwa tegemezi”alisema Tuppa.
Anaongeza”Nampongeza
Docta Chacha anaeishi Marekani kwa kuikumbuka nchi yake na kuja kuwekeza
nyumbani kwa kuanzisha kituo cha kulelea watoto yatima na watoto hao wanapata
elimu ya shule ya msingi inatotolewa kituoni,kwahiyo tunategemea kupata wasomi
wengi hapo baadae kutoka kituo cha yatima CITY OF HOPE natoa wito kwa Watanzania wengine kusaidia
katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo”alisema.
RC Tuppa
aliwaasa yatima kusoma kwa bidii licha yakuwa hawana wazazi na kuwa wajitambue
kuwa wao pia ni sehemu muhimu katika jamii nakwamba endapo watatoa fikra kuwa
wao ni watoto yatima watajijengea maisha mazuri baadae kwani wengine
watajitegemea kutokana na elimu walioipata shuleni.
“Watoto
yatima na wamazingira magumu wasijichukulie kuwa ni watoto yatima,sisi
Watanzania ndiyo walezi wenu sisi ni wazazi wenu msiwe wanyonge na mnapaswa
kupata mahitaji yote kama binadamu wengine sisi ndiyo tunawaondoa uyatima
msikubali kuitwa yatima kwa sababu wananchi wote wa Mkoa wa Mara ndiyo wazazi
wenu mkitoa fikra kuwa ninyi si watoto yatima mtajijengea maisha mazuri.
Mwanzilishi
wa kituo hicho cha watoto yatima Docta John Chacha anasema kuwa pamoja na
kuanzisha kituo hicho wanakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile upungufu
wa vitabu,madawa katika kituo cha kutolea huduma ya afya kituoni hapo na ukosefu
wa madactari ambapo ameiomba Serikali kukisaidia kituo katika kuwapatia Wauguzi
na madawa kwa ajili ya huduma ya tiba kwa watoto.
Docta Chacha
alisema kuwa kituo hicho cha watoto yatima kinahudumia jumla ya watoto 416
ambao pia wanapata elimu kuanzia darasa la awali hadi darasa la saba na
inawalimu wapatao 15 wakiume wakiwa 9 na wakike 6 nakuwa kwa mwaka huu kwa mara ya kwanza
watahitimu wanafunzi darasa la saba
wapatao 8 wavulana wakiwa 6 na wakike 8.

No comments:
Post a Comment