WATU watatu wa familia moja wamefariki dunia baada ya
kugongwa na gari katika kijiji cha Kusenye Kata ya Suguti katika
halmashauri ya Musoma vijijini mkoani Mara
Afisa Mtendaji wa kata ya Suguti Bw Jackson Marwa
akiongea kwa njia ya simu kuwa
ajali hiyo imetokea juzi majira ya jioni.
Amesema ajali hiyo inadaiwa kusababishwa na gari yenye
namba za usajili T 752 BQR iliyokuwa ikiendeshwa na Bw Anthony Kusaga
wakati akitokea Manispaa ya Musoma kwenda katika kijiji cha Saragana.
Amesema ajali hiyo imesababishwa na mwendo kasi na
hivyo kushindwa kuimudu wakati alipokuwa katika kona karibu na ya zahanati ya
kijiji hicho.
Hata hivyo afisa mtendaji huyo amewaja watu waliokufa
katika ajali hiyo ni Regina Mwelo mwenye umri wa mika 5,Nyakwesi Mwelo mwenye
umri wa miaka 15 na Asha Mwelo mwenye umri wa miaka 17.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mara Kamisha
msaidizi Mwandamizi Abslom Mwakyoma amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na
kwamba Jeshi la Polisi linamshikilia dereva wa gari hilo
.................................
WATATU WAUWAWA NA WANANCHI WENYE
HASIRA KALI.
Dinna Maningo,Tarime
WATU watatu WAKAZI WA Kijiji cha
magena kata yaTurwa Wilayani Tarime Mkoani Mara wamewauwa kwa kupigwa hadi
kufa na wananchi wenye hasira kali kwa madai ya kuhusika na wizi wa ng’ombe .
Akiongea na Waandishi wa habari
ofisini kwake Kamanda wa polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Justus
Kamugisha alisema kuwa watu waliouwawa wanatuhumiwa na wananchi kwa
kujihusisha na wizi wa mara kwa mara kijijini hapo ambapo wananchi
walijichukulia sheria mkononi kuwauwa kwa madai ya kuiba ng’ombe.
Kamanda kamugisha alisema kuwa
tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 6 .30 usiku huko kalibu na Mto
Nyamiobo katika kijiji cha Magena ambapo aliwataja waliouwawa
kuwa ni Ndiege Nyamhanga {25} Mang’iti Kamunu{30} na Nyaikore Simion {42}.
Alisema kuwa watu hao waliuwawa
kwa kushambuliwa kwa silaha za jadi na kisha kuwachoma moto nakwamba chanzo
cha mauwaji hayo ni wananchi kuwatuhumu watu hao kuiba ng’ombe ambapo miili
ya marehemu imefanyiwa uchunguzi kwa mazishi na kuwa juhudi za kuwasaka
waliohusika na tukio hilo zinaendelea.
Kamugisha aliwaasa wananchi
kutojichukulia sheria mkononi kwa watu wanaowatilia mashaka na badala yake
watoe taarifa katika vituo vya polisi ili sheria zichukuliwe dhidi yao.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
|
RORYA
SERIKALI
imedaiwa kupuuza maelekezo na ushauri wa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabe za
serikali ya kutaka kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria,maafisa
kadhaa waandamizi wa halmashauri ya wilaya Rorya mkoani Mara kwa tuhuma za
ufisadi badala yake imewahamishia vituo vipya vya kazi.
Maafisa hao
ambao wamehamishia katika vituo vipya vya kazi na katika halmashauri za
Kiteto,Rukwe,Karagwe,Kwimba na Mafia pamoja na makao makuu ya mkoa wa Morogoro
ilipendekezwa na ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali
katika taarifa yake ya ukaguzi maalum ya machi 2011 kuwa maafisa hao wasimamishwe
kazi na kufikishwa katika vyombo vya dola.
Kwa mujibu wa
taarifa hiyo ya CAG,maafisa walikuwa wa wilaya ya Rorya ambao walipaswa
kuchukuliwa hatua za kisheria kwa tuhuma za kusababisha ubadhilifu wa zaidi ya
milioni 200 ikiwa ni pamoja na kutumia madaraka vibaya ni aliyekuwa
mkurugenzi,mweka hazina,afisa raslimali watu mwandamizi,mhandisi wa ujenzi
wilaya,afisa mipango wilaya na afisa ugavi daraja la pili.
Kufuatia hatua
hiyo ya serikali ya kuwapangia vituo vipya vya kazi watumishi hao licha ya CAG
kubaini kuwa wana tuhuma za kujibu,baadhi ya madiwani wa CCM katika
halmashauri ya Rorya,wametangaza kuwa endapo serikali itashindwa kuchukua hatua
ndani miezi mitatu kuanzia sasa wako tayari kukiama chama chao katika
kuwatendea haki wananchi.
Hata hivyo ripoti
hiyo ya CAG imeipendekeza kwa baadhi ya watumishi kupewa adhabu ya kalipio
kali,kuonywa na kukatwa mishahara yao kulingana na makosa waliyobainika
kuyafanya.
Kwa mujibu wa
taarifa hiyo wtumishi wa kundi lilitakiwa kufikishwa katika vyombo vya sheria
ni Bw Edwin Nyamsekela,Bw Chacha Moseti,Bw Alex Bw Albinus na Samwel Coyhuku
CAG akipendekeza kesi ikianza itabidi watumishi hao wasimamishwe kazi mpaka
kesi itakapomalizaka.
No comments:
Post a Comment