Raia wa Venezuela wamemlaki kwa shwangwe Rais Hugo Chavez, aliyerejea kama shujaa kutoka Cuba alikokwenda, kufanyiwa matibabu.
Ilikuwa ni shangwe na vifijo, jijini Caracas hapo jana, wakati kiongozi wa taifa hilo, akiwahutubia wananchi wake, mara tu baada ya kufanyiwa upasuaji jijini Havana.
Maelfu ya raia walikusanyika ikulu, kumuona Rais Chavez, ambaye amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa takriban mwezi mmoja sasa.
Maelfu ya raia walikusanyika ikulu, kumuona Rais Chavez, ambaye amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa takriban mwezi mmoja sasa.
Tarehe nane, mwezi uliopita, kiongozi huyo aliondoka nchini humo kuelekea Cuba, na siku mbili zilizofuata hali yake ya kiafya ilikuwa mbaya, jambo lililozua minong'ono mingi, ikihoji uwezo wa Chavez, kuongoza taifa la Venezuela.
Chanzo rfi
No comments:
Post a Comment