Dinna Maningo,Tarime.
KIKUNDI cha Tembo Mazingira kinachojishughulisha na
kilimo cha mazao ya chakula na biashara pamoja na uoteshaji wa miche kilichopo kijiji cha Nyabitocho kata ya Mbogi
Wilayani Tarime Mkoani Mara kimesema kuwa kinategemea kupata mazao mengi baada
ya Halmashauri ya Wilaya ya Tarime
kukipatia trecta yenye thamani ya milion
44,207,000 kwa ajili ya shughuli za kilimo.
Wameyasema hayo wakati wakikabidhiwa trecta na Mkuu wa
Wilaya ya Tarime John Henjewele ambaye
alikuwa mgeni rasmi ,wanakikundi hao
wamesema kuwa trecta hiyo itarahisisha shughuli zao za kilimo kwani itatumika kubeba mazao, mbolea na kulima
ambapo kwa muda mlefu wamekuwa wakilima kwa kutumia majembe ya mkono (plau).
Afisa
kilimo wa Wilaya ya Tarime Selvanus Gwiboha
amesema kuwa kikundi cha Tembo kiliibua mradi wa trecta ambao uliingizwa kwenye
bajeti mwaka 2010/2011 ambapo jumla ya 55,000,000 ilitengwa kwa shughuli hiyo na kwa robo ya nne ya mwaka wa fedha
2011/12 trecta hilo limenunuliwa kwa thamani ya milioni 44,207,000 ikiwa na tela, jembe la
kulimia na la harrow na kikundi kiliweza
kuchangia asilimia 20% milioni
11,000,000 na kuweza kupata trecta kupitia mradi wa DADP.
Mkuu wa
Wilaya John Henjewele aliyekuwa mgeni rasmi kwa kuwakabidhi trecta amewataka
wanakikundi kuonyesha nidhamu umoja na mshikamano katika shughuli mbalimbali za
kikundi ili wapate mapato mengi katika
shughuli zao za kilimo.
WANANCHI MTAA WA STAREHE
KUKUMBWA NA MAFURIKO.
Dinna Maningo,Tarime.
WANANCHI wa Mtaa wa starehe
mjini Tarime wameiomba Serikali kufukia korongo la starehe ambalo limekuwa kero
kwao kwa muda mrefu nakwamba endapo lisipofukiwa huwenda kukatokea maafa makubwa
hasa kwa kipindi hiki cha mvua ya erinino.
Wakiongea na VFM wamesema kuwa kutokana na
kuwepo kwa mvua kubwa zinazoendelea
kunyesha hivi sasa kuna hatari nyumba zilizopo kando kando mwa korongo
zikabomoka baada ya korongo hilo kujaa maji.
Mwenyekiti wa Mtaa wa starehe Genkuru Tagaya (CCM) amesema kuwa kwa muda
mrefu tangu mwaka 2005 korongo hilo limekuwa likipigiwa kelele na viongozi wa mtaa lakini hakuna hatua zozote za Seikali zilizochukuliwa ili kuwanusuru wananchi waishio pembezoni mwa korongo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Tarime Fidelis Lumato amesema kuwa
korongo hilo ni kubwa sana na linahitaji kiasi kikubwa cha pesa ili kuboresha
na hivyo Halmashauri haina pesa
kwa sasa kwakuwa korongo hilo
halikutengewa bajeti yake na hivyo kuwataka kuwa na subira katika kipindi
kingine cha bajeti.
No comments:
Post a Comment