JESHI LA POLISI MUSOMA NGANGARIIIIIIII
ASKARI wa Jeshi la Polisi Kituo cha kati Musoma wakiwaonesha waandishi
wa habari dawa za kulevya aina ya Mirungi iliyokamatwa, pamoja na dawa
za Binadamu aina ya Alu, Amoxiline, Dawa za usingizi, SP, Qunin Syrup,
dawa za Kifua Kikuu kutoka nchini Kenya kuingia nchini kupitia sirari
wilayani Tarime katika kampuni tofauti za mabasi ya Zacharia na Batico
zikiwa zimehifadhiwa kwa mbinu mpya mithili ya mafuta ya kupikia,
Kulia ni Mkuu wa Kituo cha Polisi kati Musoma, Babu Sanare. (Picha na Thomas Dominick)
Majaji katika mahakama maalum
kuhusu vita nchini Sierra Leone, leo watatoa hukumu dhidi ya aliyekuwa
Rais wa Liberia Charles Taylor kwa kuhusika na vita hivyo vilivyodumu
miaka 10.
Kiongozi huyo wa zamani anadaiwa kufadhili waasi wa RUF.
Zaidi ya mashaidi 100 wamefika mbele ya mahakama hiyo lakini Bw Taylor amekanusha kuhusika na uhalifu huo wakivita na anadai kuwa kesi hiyo ni njama ya kummaliza kisiasa.
Hukumu ya majaji hao inasubiriwa kwa hamu sana na raia nchini Sierra Leone ambao jamaa zao waliathirika sana wakati wa vita hivyo.
Inakadiriwa kuwa zaidi wa watu elfu 50 waliuawa na wengine wakiwemo wanawake na watoto walibakwa na kukatwa mikono au miguu na waasi wa RUF ambao upande wa mashtaka unasema walipata usaidizi wa silaha kutoka kwa Bw Taylor.
Wakati wa vita hivyo, mwendesha mashtaka anasema kuwa Taylor alikuwa kiungo muhimu katika biashara haramu ya almasi kutoka Sierra Leone.
Kesi hii iliodumu miaka mitatu na nusu, hata hivyo huenda isi kamilike leo kwani pande zote wanauhuru wa kukata rufaa ikiwa hukumu hiyo haitawaridhisha.